Home Makala Yanga sc Yakomaa na Mbrazil wa Singida Big Stars

Yanga sc Yakomaa na Mbrazil wa Singida Big Stars

by Dennis Msotwa
0 comments

Taarifa za ndani zinadai kuwa klabu ya Yanga sc inaweza kubadilishana wachezaji Jesus Moloko na Mbrazil Dario Federico da Silva anayeichezea Singida Big Stars ambayo imepanda kushiriki ligi kuu nchini.

Mabosi wa klabu ya Yanga sc wamefanikiwa kumuona Dario mara mbili wakati akiichezea klabu hiyo katika michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Zanaco Fc ya Zambia na dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo wamevutiwa na uwezo wake hivyo wanataka ajiunge kikosini mara moja huku wakiwapa Singida Big Stars mchezaji Jesus Moloko na kiasi cha pesa.

Bosi mkubwa kabisa wa Singida United ni mshabiki mkubwa wa klabu ya Yanga sc na ameshafanya hivyo kwa kuwapa Yanga sc mchezaji Feisal Salum na Ally Mtoni Sonso licha ya kuwa Feisal tayari alikua amesajiliwa na Singida United wakati huo.

banner

Taarifa ya mitandao ya kijamii ya Singida Big Stars imekanusha kuwepo kwa dili hilo lakini inasemekana hiyo ni geresha kwani tayari mazungumzo yamefikia mbali katika dili hilo na linaweza kukamilika muda wowote.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited