Home Makala Yanga sc Yapaa Algeria

Yanga sc Yapaa Algeria

by Dennis Msotwa
0 comments

Kikosi cha wachezaji wa Yanga pamoja na viongozi kimeanza safari ya kuelekea nchini Algeria alfajiri ya leo kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya CR Belouizdad utakaofanyika siku ya Novemba 24 nchini humo.

Kikosi hicho ambacho kimesafiri asubuhi ya leo kimejumuisha mastaa wale ambao hawapo katika timu za taifa huku wengine wenye majukumu ya mechi ya kimatifa na timu za taifa wanarajiwa kuungana na kikosi siku moja kabla ya mchezo.

Mastaa kama Stephane Aziz Ki,Djigui Diarra na Khalid Aucho wenyewe wataunganisha ndege juu kwa juu huku wale walioko na kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania wakitarajiwa kuondoka mapema kesho baada ya mchezo wa leo usiku baina ya Tanzania na Morocco.

banner

Max Nzengeli,Pacome Zouzou,Jonas Mkude ni moja ya mastaa walionekana katika msafara wa klabu hiyo kuelekea nchini Algeria tayari kuzisaka alama tatu za hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited