Home Makala Yanga sc,Morrison Wamalizana

Yanga sc,Morrison Wamalizana

by Sports Leo
0 comments

Taarifa za kuaminika kutoka kwenye vyanzo mbalimbali zinasema kuwa, klabu ya Dar Young Africans imemalizana na nyota wake wa zamani raia wa Ghana, Bernard Morrison kwa ajili ya kupata huduma yake kwenye msimu ujao katika michuano mbalimbali.

Morrison ambaye hivi karibuni alitangazwa kupewa likizo ya hadi mwisho wa msimu na klabu yake ya Simba na taarifa za sasa kuripoti kuwa amemalizana na klabu ya Yanga huenda akawepo kama mtazamaji kwenye mchezo wa Nusu Fainali ya FA inayotarajiwa kuzikutanisha timu za Simba na Yanga ndani ya dimba la CCM Kirumba Mwanza.

Mpaka sasa licha ya kupewa mapumziko ya muda usiojulikana na klabu yake ya Simba sc lakini mchezaji huyo mpaka sasa bado hajasafiri kuelekea nchini Ghana ambapo inasemekana yupo nchini huku akiwa hapokei simu za waajiri wake klabu ya Simba sc na tayari ameanza mazungumzo ya kurudi Yanga sc klabu ambayo ilimleta hapa nchini.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited