Leo Agosti Mosi, Yassin Mustapha amesaini dili jipya la kuitumikia Yanga akitokea Polisi Tanzania iliyokuwa ikinolewa chini ya Malale Hamisi.
Yassin Mustapha anakuwa ni wa tatu kutambulishwa rasmi ndani ya kikosi cha Yanga, wa kwanza akiwa ni Zawadi Mauya kutoka Kagera Sugar akifuatiwa na Bakari Mwamnyeto kutoka Coastal Union.