Home Makala Yanga,Gsm Wazidi Kunoga

Yanga,Gsm Wazidi Kunoga

by Sports Leo
0 comments

Mkurugenzi wa uwekezaji kutoka GSM Eng. Hersi Said amekiri kuwa tayari kampuni ya GSM wamesaini mkataba na klabu ya Yanga Sc kwa ajili ya kutengeneza bidhaa za klabu (Club Merchandise) ambazo zitakuwa na chapa ya Yanga Sc.

Mkataba huo kati ya Yanga Sc na GSM utaipa fursa kampuni ya GSM kutumia chapa ya Yanga kutengeneza bidhaa nyingine tofauti na jezi. Bidhaa hizo ni kama truck suits, t-shirts, vikombe,saa, viatu , bracelets, na nyingine nyingi ambazo zitatengenezwa.

Eng. Hersi ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano katika kituo cha Azam Tv kupitia kipindi cha michezo cha Mshike Mshike Viwanjani.
Hii ni moja ya njia ambayo itaongeza mapato ya Klabu ya Yanga Sc kutokana na mauzo yatokanayo na bidhaa hizo zitakazo zalishwa na kampuni hiyo ambapo Mashabiki na Wanachama wa Yanga Sc wataweza kununua bidhaa hizo kuanzia msimu unao kuja (2021).

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited