Home Makala Zahera Njia Panda Yanga

Zahera Njia Panda Yanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Kutokana na usajili wa nguvu uliofanyika Jangwani kocha Mwinyi Zahera ameanza kupata mtihani wa kupanga wachezaji baada ya wengi kuonekana kupania kuingia kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

Golini kiwango kilichooneshwa na kipa Metacha Mnata  katika mechi dhidi ya Township Rollers ambapo kipa huyo alidaka penati kimemfanya kocha huyo kupata wakati mgumu wa kuamua nani aanze katika mechi ya ufunguzi leo dhidi ya Ruvu shooting ambapo umahiri wa kipa namba moja Farouk shikalo unajulikana na kufanya kocha Zahera aumize kichwa.

Upande wa mabeki pacha ya Yondani na Lamine inaonekana kukubalika japo pia uwepo wa Ally Mtoni na Mustapha Selemani unafanya kocha huyo kupasua kichwa japo kwa upande wa mabeki wa pembeni kuna unafuu kutokana na majeruhi ya Paulo Godfrey na Ally Ally.

banner

Safu ya viungo imeshikwa na Mohamed Issa na Papy Tshitshimbi huku Mapinduzi Balama na Patrick Sibomana wakitokea pembeni japo majeruhi ya Mohamed Issa yatampa nafasi ya kuamua kati ya Feisal Salum na Abdulazizi Makame.

Nafasi ya ushambuliaji Juma Balinya na Sidney Urikhob wana nafasi ya uhakika mbele ya Issa Bigirimana japo uwepo wa David Molinga unatishia uhai wa pacha hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited