Home Makala Zaidi Ya Milioni 417 Yagharimu Ligi Kuu

Zaidi Ya Milioni 417 Yagharimu Ligi Kuu

by Sports Leo
0 comments

Mechi zilizosalia za ligi kuu Tanzania Bara zitagharimu zaidi ya Sh 417 milioni ambazo zitatumika katika uendeshaji kwa timu na malipo ya posho kwa waamuzi na maofisa wengine wanaosimamia michezo ya Ligi Kuu.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amesema kuwa tathmini iliyofanywa na timu ya wataalam wa wizara yake imeonyesha kuwa kiwango hicho cha fedha kinahitajika ili kuweza kumalizia ligi hiyo iliyobakiza raundi 9 (mechi 93).

Waziri amesema kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Bodi ya Ligi Kuu (TPLB), klabu pamoja na wadhamini wanalo jukumu la kuona wanamudu vipi gharama hizo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited