Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imemfungia Mchezaji wa Klabu ya Simba SC, Ibrahim Ame Mohamed michezo mitatu (3) na faini ya Tsh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumzuia Mwamuzi msaidizi wa mchezo kufanya kazi yake.
Tukio hilo lilitokea katika mchezo kati ya Simba Sc na Gwambina FC uliochezwa Aprili 24, 2021 kwenye uwanja wa Gwambina mkoani Mwanza.
Mwamuzi huyo, Godfrey Msakila ameondolewa katika ratiba ya waamuzi kwa mizunguko mitatu (3) kwa kosa la kushindwa kumudu mchezo huo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Katika Mechi hiyo hiyo, Simba SC imetozwa faini ya Tsh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la Mashabiki wake kurusha chupa tupu na zenye maji uwanjani na kusababisha mpira kusimama kwa zaidi ya dakika hadi Polisi kuingilia kati kutuliza ghasia hiyo.