Home Soka Arsenal yanasa kitasa cha Brighton

Arsenal yanasa kitasa cha Brighton

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na klabu ya Brighton and Hove Albion kumsajili beki wa kati Muingereza Ben White kwa ada ya paundi milioni 50.

Ben aliitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya England kwenye michuano ya Euro 2020.

Beki huyo alicheza kwa kiwango kikubwa akiwa kwa mkopo Leeds United na kuisaidia kupanda daraja msimu wa 2020/2021 hali iliyopelekea klabu yake mama ya Brighton kumrudisha na kumpa mkataba wa miaka minne.

banner

Brighton ilikataa ofa mbili za Arsenal kutokana na Ben kuzivutia timu nyingine kubwa kama Everton na Man Utd, Mchezaji huyo kwasasa yup mapumzikoni hivyo atafanyiwa na kutambulishwa atakaporudi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited