Home Soka Aussems Akalia Kuti Kavu

Aussems Akalia Kuti Kavu

by Sports Leo
0 comments

Imeelezwa kuwa kocha mkuu wa klabu ya Simba sc Patrick Aussems amepewa onyo na uongozi wa klabu hiyo kuhusiana na mwenendo wa timu hiyo ambao haujawaridhisha viongozi na mashabiki wa klabu hiyo.

Chanzo chetu kutoka ndani ya klabu hiyo kinaeleza kwamba kocha huyo amekua na urafiki na baadhi ya mastaa katika timu hiyo kiasi cha kuleta masihala katika kazi.

Taarifa zilizo chini ya kapeti zinasema, Kocha huyo ambaye ni raia wa Ubelgiji ameambiwa apunguze urafiki na wachezaji ili kufanikisha malengo yake.

banner

Inaelezwa kuwa Aussems amekuwa na urafiki zaidi na wachezaji wa Simba kiasi cha kwamba kitendi hicho kinapelekea ashindwe kutimiza majukumu yake kisawasawa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited