Home Soka Azam FC,Biashara Utd wajua wapinzani wao CAF

Azam FC,Biashara Utd wajua wapinzani wao CAF

by Sports Leo
0 comments

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kombe la shirikisho la vilabu barani Afrika timu za Azam na Biashara Mara ambazo zimefanikiwa kufuzu hatua ya pili ya mtoano zitakabiliana na wapinzani kutoka Misri na Libya.

Chama cha soka Afrika wametoa ratiba ya michezo ya raundi hiyo ambapo Azam amepangiwa kucheza na Pyramids ya Misri huku wanajeshi wa mapakani Biashara United itakabiliana na Al Ahly Tripol ya Libya.

Timu zote mbili zitaanza michezo ya kwanza nyumbani inayotarajiwa kupigwa kati ya tarehe 15-17 mwezi Oktoba huku michezo ya marudiano ikipangwa kuchezwa kuanzia Oktoba 22-24 mwaka huu.

banner

Azam FC walifanikiwa kusonga mbele baada ya kuwafunga klabu ya Horseed ya Somalia kwa jumla ya mabao 4-1 kwenye michezo miwili huku Biashara wakivuka kwa ushindi wa jumla wa magoli 3-0.

Wawakilishi wengine wa Tanzania Simba SC katika michuano ya klabu bingwa wao watamenyana na Jwaneng FC kutoka Botswana katika hatua ya pili kufuzu makundi ya michuano hiyo.

Kufanya vizuri kwa vilabu hivyo kutaiongezea alama Tanzania na kuiwezesha kuendelea kupeleka wawakilishi wanne katika mashindani ya CAF.

Ratiba kamili ni kama ifuatavyo;

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited