Home Soka Bajana,Ndoye Kutibiwa Afrika Kusini

Bajana,Ndoye Kutibiwa Afrika Kusini

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Azam Fc imetangaza kuwa mastaa wake wawili Sospeter Bajana na Malickou Ndoye wataondoka kwenda nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya matibabu ya nyonga katika hospitali ya Vicent Palloti iliyopo jijini Cape Town nchini humo.

Mastaa hao walimia kwa nykati tofauti tofauti katika michezo ya ligi kuu ambapo baada ya tathmini ya kina wameonekana kuwa wanastahili kupatiwa matibabu katika Hospitali hiyo.

Taarifa iliyochapishwa kutoka katika mitandao ya kijamii ya klabu hiyi ilisomeka kuwa “Wachezaji wetu wawili, @sospeter_bajana04 na @malickou_ndoye, wanatarajia kuondoka nchini Februari 20, mwaka huu, kuelekea jijini Cape Town, Afrika Kusini kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa majeraha yao”.

banner

Bajana ambaye ni nahodha wa zamani wa klabu hiyo ni tegemeo hasa klabuni hapo katika eneo la kiungo huku Ndoye ambaye husumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara yeye amekua na wakati mzuri pindi anapopata nafasi eneo la ulinzi.

Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu nchini Azam Fc wapo katika nafasi ya tatu wakiwa na alama 32 baada ya kucheza michezo 14.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited