Home Soka Beki Lipuli Kutua Simba sc

Beki Lipuli Kutua Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Mabingwa mara tatu mfululizo wa VPL, Simba SC wamefikia hatua nzuri ya kumsajili beki wa kulia wa Lipuli, David Kameta kwa mkataba wa miaka miwili.

Msimu huu Kameta ameifungia Lipuli magoli mawili na asisti sita, akionyeshwa kadi sita za njano na moja nyekundu huku akitarajiwa kwenda msimbazi kuwa mbadala wa Shomari Kapombe anayesumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara.

Hivi karibuni Afisa Mtendaji mkuu wa klabu ya Simba sc Senzo Mbatha Mazingisa alisikika akisema kuwa klabu hiyo ina mpango wa kusajili wachezaji wachache wenye tija huku ikitema mastaa wasiopungua watano.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited