Home Soka Boxer,Balama Kuwakosa Zesco

Boxer,Balama Kuwakosa Zesco

by Dennis Msotwa
0 comments

Makinda wa Yanga Paulo Godfreyc”boxer” na Balama Mapinduzi wapo kwenye hatihati ya kuukosa mchezo wa marudiano dhidi ya Zesco united ya Zambia baada ya kukumbwa na majeraha.

Boxer aliumia katika mechi ya kirafiki jijini Arusha na mpaka leo bado hajapona akiwa tayari kashakosa mechi ya ligi dhidi ya Ruvu shooting huku akikosa mechi ya awali dhidi ya Zesco na kuna uwezekana mkubwa wa kuukosa mchezo wa marudiano huku kwa upande wa Balama yeye akiendelea kuuguza majeraha aliyopata katika mchezo dhidi ya Zesco ambapo alicheza nafasi ya beki wa pembeni kuziba pengo la Boxer.

Hata kukosekana kwa wachezaji hao hakuwezi kumpasua kichwa kocha Mwinyi Zahera kutokana na kurejea kwa Juma Abdul huku pia Ally Ally akiwa tayari kucheza nafasi hiyo.

banner

Yanga italazimika kushinda mchezo huo ama kutoa sare ya kuanzia mabao 2 na kuendelea ili kupata nafasi ya kufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited