Home Soka Chama Amponza Kigogo Yanga

Chama Amponza Kigogo Yanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Mtendaji mkuu wa klabu ya Simba sc Senzo Mazingisa amesema atamshtaki makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Fredrick Mwakalebela Baada  kusema kuwa Yanga wameanza mazungumzo na nyota wa Klabu ya Simba Clatous Chama.

Mtendaji mkuu wa Klabu ya Simba, Senzo Mazingisa ameshangazwa na Kauli hiyo na amesema atawashitaki TFF au FIFA.

Senzo amesisitiza Kama kiongozi huyo alikuwa anaongea kuwafurahisha mashabiki wake itamutokea puani kwa kuwa mchezaji huyo ni mali ya Simba na ana mkataba.

Pia Senzo ameshangaa kuona Kiongozi mkubwa wa Yanga akiongea kwenye media bila wasiwasi akijadai ameongea na Chama ni Kosa kubwa kutangaza kwenye vyombo vya habari umeongea na mchezaji ambaye ana mkataba na Klabu yake huo ni ushahidi tosha wa kumshitaki mtu/klabu kokote.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited