Home Soka Chasambi Rasmi Simba Sc

Chasambi Rasmi Simba Sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imemtambulisha rasmi kinda Ladack Chasambi kutoka Mtibwa Sugar kuwa mchezaji wa klabu hiyo baada ya kufanikiwa kununua mkataba wake uliosalia katika klabu ya Mtibwa sugar ambapo sasa atakua mchezaji wa klabu hiyo kwa miaka mitatu.

Chasambi mchezaji bora wa ligi ya vijana wa miaka 20 kwa miaka miwili mfululizo amejiunga na Simba sc baada ya klabu hiyo kulipa kiasi cha Tsh.75 milioni zilizoko katika kipengele cha kununua mkataba wa mchezaji huyo katika klabu yake ya zamani ya Mtibwa Sugar ambayo ilimpandisha kutoka timu za vijana za klabu hiyo.

Tayari baada ya kutambulishwa mchezaji huyo ameungana na kikosi cha klabu hiyo katika michuano ya kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar ambapo ameanza mazoezi rasmi akisubiri kama atapangwa na kocha Abdelhack Benchika katika michezo inayofuata Visiwani humo.

banner

Hii si mara ya kwanza kwa Simba sc kufanya biashara ya wachezaji na Mtibwa sugar ikikumbukwa kuwa iliwahi kuwasajili Salim Mbonde,Mzamiru Yassin,Mohamed Ibrahim na wengineo kuja kuhudumu klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited