Mechi iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka duniani baina ya Chelsea na Liverpool imeshindwa kupata mbabe baada ya timu hizo kutoshana nguvu kwa kufungana mabao 2-2.
Liverpool ndio waliokuwa wa kwanza kupata mabao yote mawili kupitia kwa Sadio Mane dakika 9 ya na Mohamed Salah dakika ya 26,kabla ya wenyeji kurejea mchezoni na kusawazisha kupitia Mateo Kovacic dakika ya 42 na Christian Pulisic dakika ya 45+1.
Katika mchezo huyo Liverpool ilimkosa kocha wake mkuu Jurgen Klopp kutokana na maambukizi ya Uviko-19 pamoja na wachezaji Thiago Alcantara,Alison Becker na Joel Matip,huku Chelsea ikiwakosa Andres Christensen na Timo Werner kwa matatizo hayo hayo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Sare hiyo imepelekea mbio za ubingwa wa ligi kuu soka nchini Uingereza kubaki za upande mmoja baada ya tofauti ya pointi kati ya vinara Manchester city na anayeshika nafasi ya pili Chelsea kuwa ni alama kumi baada ya michezo 21.