Home Soka Corona Yaishtua Caf

Corona Yaishtua Caf

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la soka barani Afrika-CAF kesho na keshokutwa(Machi 14 na 15,2020) Litaitembelea Cameroon ambao ni Mwenyeji wa mashindano ya wachezaji wanaocheza ligi za ndani barani Africa-CHAN.

Pamoja na mambo mengine shirikisho hilo litaangalia namna Cameroon ilivyojipanga kupambana na virusi hatari vya Corona ambavyo vimekuwa tishio katika mataifa mengine ulimwenguni pia kufanya tathmini kama mashindano hayo yafanyike au la.

Kwa mujibu wa shirika la Afya duniani-WHO,Mpaka sasa nchi 17 barani Afrika zimethibitisha kuwa na visa 160 vya virusi vya ugonjwa wa CORONA tangu ugonjwa huo ulipuke mwishoni mwa mwaka jana nchini CHINA mojawapo ikiwemo Cameroon ikiwa na visa viwili

banner

Mashindano ya CHAN yamepangwa kuafnyika kuanzia Aprili 4-25,2020 ambapo Tanzania ni moja ya timu zilizofuzu kushiriki michuano hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited