Home Soka Dube Atinga TFF

Dube Atinga TFF

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji Prince Dube ameenda katika shirikisho la soka nchini (TFF) akiwasilisha malalamiko yake akidai kwamba hatambui mkataba wake na klabu ya Azam Fc ambayo inadai kuwa ana mkataba wa miaka miwili na nusu na klabu hiyo.

Kwa mujibu wa Dube yeye anasema kuwa ana mkataba na klabu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu huu ambapo mkataba mpya wa miaka miwili ambao klabu hiyo inadai kuwa ilimsainisha kuwa hautambui na wala hajawahi kuusaini.

Malalamiko hayo ya Dube yanafanana kabisa na yale ya Benard Morrison ambaye aliukana mkataba wake na klabu ya Yanga sc na kufanikiwa nia yake kujiunga na klabu ya Simba sc ambayo ilimuwekea dau nono tofauti na lile la Yanga sc.

banner

Azam Fc yenyewe inadai kuwa ina mkataba na staa huyo mpaka mwaka 2027 ambapo alisaini mkataba mpya mwishoni mwa msimu uliopita mkataba wa miaka miwili na kufanya jumla awe na mkataba wa miaka miwili na nusu.

Azam Fc ilitangaza kukaribisha ofa za vilabu mbalimbali vyenye nia ya kumsaini staa huyo lakini licha ya vilabu vya Simba sc na Al Hilal ya Sudan kujitokeza inadaiwa kuwa bado mchezaji huyo alikataa ofa hizo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited