Imeelezwa kuwa, uongozi wa Arsenal umeanza mchakato wa kumtafuta mrithi wa kuchukua mikoba ya kocha wao wa sasa, Unai Emery ambaye amekuwa na mwendo wa kusuasua ndani ya Ligi Kuu England.
Kumekuwa na presha kubwa ndani ya Bodi ya Uongozi wa Arsenal baada ya kocha huyo wikiendi iliyopita wakiwa nyumbani kuiongoza Arsenal kulazimisha sare ya mabao 2-2 kwenye mchezo wao wa ligi hiyo dhidi ya Southampton.
Habari zinaeleza kuwa, licha ya Unai kupewa muda wa kurejesha makali ya kikosi hicho cha Arsenal, bado hawajaridhishwa na mwendo wake hivyo kinachofuatia kwa sasa ni kupigwa chini jumla.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.