Home Soka Fcc Yaijibu Simba sc

Fcc Yaijibu Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Tume ya ushindani wa kibiashara Tanzania(Fcc) imejibu shutuma zilizotolewa na Bilionea Mohamed Dewji anayetaka kuwekeza katika klabu ya Simba sc.

Fcc imekanusha taarifa za kuchelewesha mchakato wa kupitia taarifa mbalimbali za uuzaji wa klabu hiyo kwa Bilionea huyo anayedaiwa kutaka kuwekeza kiasi cha Shilingi Bilioni 20 za kitanzania.

Katika Taarifa yake kwa umma tume hiyo imebainisha kwamba imekua ikipata mrejesho mdogo kutoka kwa klabu hiyo na tayari imeshawapatia mrejesho ambao wanatakiwa kujibu ili kuendelea na hatua zingine za mchakato huo.

banner

Hivi karibuni wakati akiongeza na waandishi wa habari bilionea huyo Mo dewji aliulizwa kuhusu mchakato huo ulipofikia na alijibu kwamba umekwama katika Tume hiyo ambayo ilipewa ili kuupitia na kuudhinisha.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited