Home Soka Fraga Anarejea..

Fraga Anarejea..

by Dennis Msotwa
0 comments

Kiungo mkabaji raia wa Brazil Gerson Fraga Vieira yupo mbioni kurejea katika klabu ya Simba sc baada ya kupona majeraha yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.

Kiungo huyo mkabaji alipata jeraha la goti wakati akiitumikia klabu hiyo ambapo alihitaji muda mrefu wa matibabu hivyo kuilazimu klabu hiyo kukaa chini kuangalia namna ya kuziba nafasi yake ambapo walikubaliana kuvunja mkataba ili apate matibabu huku akirejea nyumbani kwao nchini Brazil.

Sasa kiungo huyo tayari amepona na hivi karibuni aliweka maneno katika mtandao wake wa instagram akisema kuwa ”Tutaonana si mrefu” hali iliyowafanya wemgi kuamini kuwa staa huyo aliyecheza na Neymar na Coutinho katika kikosi cha vijana timu ya Taifa ya Brazil kuwa anaweza kurejea nchini kujiunga na klabu yake hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited