Home Soka Gomez apigwa stop kukaa benchi

Gomez apigwa stop kukaa benchi

by Sports Leo
0 comments

Shrikisho la soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya makocha ambao hawaruhusiwi kukaa katika benchi la ufundi katika michuano ya klabu bingwa na ila ile ya kombe la shirikisho kutokana na kukosa sifa zinaruhusiwa kikanuni.

Kwa mujibu wa kanuni za CAF makocha wakuu wanapaswa kuwa na leseni ya CAF A kwa wale waliosomea ndani ya Afrika pamoja na UEFA pro license kwa wale waliochukua mafunzo ya ukocha barani Ulaya.

Kocha wa Simba sc Didier Gomez ana leseni ya UEFA A hivyo hana sifa za kukaa katika benchi kwa mechi zilizo chini ya CAF,Simba pia itamkosa kocha wake msaidizi Suleiman Matola ambaye hana leseni ya CAF B inayomuwezesha kuwepo kwenye benchi la ufundi.

banner

Makocha wengine waliopigwa marufuku hiyo ndani ya Afrika Mashariki ni pamoja na kocha wa KMKM ya Zanzibar Ame Khamis,kocha wa APR ya Rwanda Erradi Mohamed Ali,Bosa Wasswa wa Express Fc ya Uganda.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited