Kocha mkuu wa klabu ya Simba Didier Gomes ameuambia uongozi wa klabu hiyo kuwa kwenye usajili wa msimu ujao anahitaji wachezaji 5 wapya wa nguvu ikiwa wachezaji wawili wa Kimataifa na watatu wakiwa wachezaji wa ndani.
Kwenye ripoti ya Gomes inaonesha kuwa anahitaji mabeki wawili (kushoto na Kati) Viungo wawili na mshambuliaji mmoja,
Kwenye ripoti hiyo Gomes anataka viungo wawili (mkabaji na mshambuliaji) pamoja na mshambuliaji mmoja wa kati mwenye uwezo wa kuwazidi akina Kagere, Mugalu na Bocco,
Pia Gomes ameishauri klabu ya Simba kuachana na wachezaji 3 wazawa na wawili wa kimataifa (mmojawapo Kahata) na ameuomba uongozi wa klabu hiyo kumtoa kwa mkopo perfect Chikwende ambapo uongozi wa klabu hiyo unafikiria kmtyafutia timu nje ya nchi.