Home Soka Hali Tete Yanga

Hali Tete Yanga

by Sports Leo
0 comments

Hali ya upepo imebadilika katika klabu ya Yanga baada ya kupata matokeo ya sare mfululizo katika mechi tatu za ligi kuu Tanzania bara.

Yanga ilianza kupata sare dhidi ya Mbeya city kisha ikatoa suluhu na Prisons na tena katika mchezo wake dhidi ya Polisi Tanzania ikatoa sare licha kuongoza kwa goli la Tariq Seif dakika ya 41.

Klabu hiyo inakabiliwa na hali tete baada ya kulazimika kwenda uwanja wa Mkwakwani Tanga kwenda kupambana na Coastal union ambaye imetoka kujeruhiwa kwa mabao 2-1 na Ruvu Shooting.

banner

Pia Yanga itakua na wakati mgumu kupambana na timu hiyo inayonolewa na Juma Mgunda ambaye ni kocha mzoefu wa ligi kuu na michuano ya kimataifa akitoka kuifundisha Taifa Stars katika michuano ya chalenji.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited