Home Soka Ivory Coast Waanza Afcon na Ushindi

Ivory Coast Waanza Afcon na Ushindi

by Sports Leo
0 comments

Wenyeji wa michuano ya mataifa ya Afrika (Afcon 2024) timu ya Taifa ya Ivory Coast imeanza vyema michuano hiyo baada ya kufanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Gambia katika mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo uliofanyika nchini humo na kuhudhuriwa na maelfu ya mashabiki.

Mabao ya Ivory Coast yalifungwa na Christian Kouamé (45′) pamoja na Seko Fofana (85′) na kupeleka kilio kwa Gambia inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga sc Tom Saintfiet ambaye ni raia wa Ubelgiji.

Ivory Coast pamoja na ushindi huo bado haikua na kiwango kilicho bora katika mchezo huo kinyume na matarajio ya mashabiki wengi waliokua na imani kuwa wenyeji hao wataonyesha soka safi kutokana na maandalizi makubwa waliyofanya.

banner

Msimamo wa kundi A sasa wenyeji wanaongoza wakiwa na alama tatu huku Nigeria na Equatorial Guinnea kila mmoja akiwa na alama moja moja na Gambia akiwa mwishoni mwa msimamo akiwa hana alama.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited