Kiungo raia wa Mali Sadio Kanoute amejiunga na mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba SC kwa mkataba wa miaka miwili kuwatumikia wekundu hao wa Msimbazi.
Kanoute alifanya vizuri katika michuano ya CHAN mwaka jana nchini Cameroon na anafunga usajili wa wachezaji wa kigeni ndani ya timu hiyo baada ya kutimia wachezaji 12 idadi inayoruhusiwa kikanuni.
Mchezaji huyo ana uwezo wa kucheza nafasi zote za kiungo wa kati.