Home Soka Kapombe Ajiengua Stars

Kapombe Ajiengua Stars

by Sports Leo
0 comments

Beki wa timu ya Simba sc Shomari Kapombe amejitoa kuichezea timu ya taifa ya Tanzania (Taifa stars) kutokana na kuandamwa na majeraha ya mara kwa mara hali inayotishia uhai wa soka lake.

Kapombe aliwasilisha barua katika shirikisho la soka nchini(Tff) kuhusiana na suala hilo ambapo barua hiyo inasomeka kuwa beki huyo amejitoa kushiriki katika timu ya taifa mpaka afya yake itakapotengemaa.

Beki huyo aliumia mwaka huu katika kambi ya timu ya taifa nchini Afrika ya kusini wakati wakijiandaa na mchezo dhidi ya Lesotho na toka aumie hajarudi fiti mpaka jana aliposhiriki mechi ya kwanza na klabu yake ya Simba katika mchezo dhidi ya Mbeya city.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited