Beki wa pembeni wa klabu ya Simba sc Shomari Kapombe amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo kwa miaka miwili zaidi baada ya ule wa awali kuelekea ukingoni.
Kapombe amesaini mkataba huo na kumaliza uvumi wa kuhitajika katika timu ya Far Rabat inayoshiriki ligikuu nchini Morroco ambayo inanolewa na kocha wa zamani wa timu ya Simba sc Sven Vandebroek.