Home Soka Kisa Simba,Azam Kocha Yanga Awa Mbogo

Kisa Simba,Azam Kocha Yanga Awa Mbogo

by Dennis Msotwa
0 comments

Kitendo cha kurejea kwa baadhi ya Mastaa wa Klabu ya Simba sc waliokua nje ya nchi huku pia kocha wa timu ya Azam fc Aristica Cioaba kimemkasirisha kocha wa Yanga sc Luc Eymael kiasi cha kuposti maneno makali kwa uongozi wa klabu hiyo.

Kocha amesema hajafurahishwa na majibu anayopewa na viongozi wa klabu hiyo kuwa ndege zimejaa baada ya baadhi ya nchi kuruhusu safari za ndege ilihali washindani wake Simba sc na Azam fc zimefanikiwa kuwasafirisha mastaa wao.

Kocha huyo aliyekwama nchini Ubelgiji alisema hayo kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter akilaumu suala hilo huku timu ikiwa imeanza mazoezi chini ya kocha msaidizi Bonifasi Mkwasa kwa kufuata maelekezo ya kocha huyo aliyeko nje.

banner

Licha ya juhudi za kuwatafuta viongozi wa Yanga sc wazungumzie suala hilo bado ilituwia vigumu kuwapata.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited