Home Soka Kitambi Atua Geita Gold SC

Kitambi Atua Geita Gold SC

by Sports Leo
0 comments

Aliyekua kocha wa zamani wa klabu za Azam Fc na Namungo Fc Dennis Kitambi amejiunga na klabu ya Geita Gold Sc akichukua nafasi ya Hemed Morroco ambaye aliamua kujiuzuru kuifundisha timu hiyo yenye makazi yake mkoani Geita.

Kitambi alikua kocha wa Namungo Fc lakini alitimuliwa baada ya timu hiyo kuwa na mwenendo mbaya ambapo sasa rasmi ametambulishwa kuwa kocha wa Geita Gold Fc.

Kitambi atakua na kazi kubwa ya kufanya kurejesha furaha kwa wakazi wa Geita baada ya timu hiyo kuwa na matokeo yasiyoridhisha katika ligi kuu nchini ambapo mpaka sasa ipo nafasi ya kumi ya msimamo ikiwa na alama 16 za ligi kuu.

banner

Hata hivyo tayari kocha huyo ameanza na ushindi katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Singida Fountain Gate Fc baada ya kushinda 1-0 goli la Valentino Mashaka dakika ya 79 ya mchezo uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Nyankumbu mkoani Geita.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited