Home Soka Klopp kwenye kashfa na Waafrika

Klopp kwenye kashfa na Waafrika

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp ni kama ameingia kwenye mgogoro na Waafrika baada ya kuyaita mashindani ya mataifa Afrika ya soka(AFCON) kuwa ni mashindano madogo.

Klopp aliyasema hayo alipokuwa kwenye mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya(Uefa champions league).

Katika mkutano huo Klopp alisema kuwa kuna mashindano madogo ya Afrika yanakuja mwezi Januari,kitu ambacho kilifanywa aulizwe na mmoja wa waandishi wa habari waliokuwepo kuwa kwanini ameyaita mashindano hayo kuwa ni madogo?

banner

Kauli hiyo imepokelewa vibaya na wadau wa soka Afrika kwani kusema hivyo ni kudhalilisha mashindano hayo ambayo ni makubwa zaidi kwa Waafrika.

Hayo yamejiri kipindi ambacho Klopp ataenda kuwapoteza wacezaji wake Mane,Salah,Matip na Naby Keita kitu ambacho huenda kikawapunguzia kasi kwenye ligi kuu soka nchini Uingereza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited