Home Soka Kmc Yamsajili Banda

Kmc Yamsajili Banda

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Kmc Fc imefanikiwa kuinasa saini ya winga Peter Banda raia wa Malawi na kuizidi kete klabu ya Singida Fountain Gate Fc ambayo ilianza mazungumzo na staa huyo mapema tangu mwishoni mwa mwaka jana.

Banda ametua Kmc baada ya Singida Fg kuchelewa kukamilisha dili hilo huku kifungo cha kuzuiwa kusajili na Fifa pamoja na TFF kikiwaponza kutokana na kushindwa kulipa fedha kwa wakati ili waepuke zuio hilo.

Banda mchezaji wa zamani wa Simba sc anakwenda Kmc kuiongezea nguvu klabu hiyo hasa katika eneo la ushambuliaji lililochini ya Waziri Junior huku timu hiyo mpaka ligi inasimama ikiwa katika nafasi ya nne ikiwa na alama 21 baada ya kucheza michezo 14 ya ligi kuu.

banner

Kmc imepanda viwango chini ya mwalimu Abduhamid Moalin kiasi cha kufanya vizuri msimu huu tofauti na msimu ulioisha.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited