Home Soka K’njaro Queens Watinga Fainali

K’njaro Queens Watinga Fainali

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya taifa ya wanawake Kilimanjaro Queens imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya chalenji baada ya kuwafunga Uganda katika mchezo wa nusu fainali uliofanyika uwanja wa chamazi jijini Dar es salaam.

Iliwalazimu mashabiki kusubiri mpaka dakika ya tisini kujua hatma ya mchezo huo baada ya Asha Rashidi “Mwalala” kufunga bao kwa shuti kali akipokea pasi ya Mwanahamisi Omary “Gaucho”.

Kilimanjaro queens itaungana na Kenya kucheza fainali siku ya jumatatu huku Uganda itakutana na Burundi kuwania mshindi wa tatu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited