Home Soka Kotei Kurudi Simba sc

Kotei Kurudi Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Kulekea katika usajili wa dirisha dogo klabu ya Simba sc ipo mbioni kumrudisha kiungo James Kotei iliyoachana nae misimu wa 2018/2019 baada ya kocha Sven Vandebroek kupitisha usajili huo.

Inadaiwa kwamba baada ya klabu hiyo kuachana na kiungo Mbrazil Gerson Fraga aliyeumia goti klabu hiyo ipo mbioni kumsajili kiungo huyo baada ya mmoja ya viongozi wa juu wa klabu hiyo kumuonyesha kocha Sven video za kiungo huyo mkata umeme ndipo kocha alikubali usajili huo.

Kotei aliondoka klabuni hapo na kujiunga na Kaizer Chiefs ya nchini Afrika ya Kusini lakini alitemwa baada ya kukosa nafasi ndipo alipojiunga na klabu ya Slavia Mozyr ya nchini Beralus alipo mpaka sasa kwa mujiubu wa mtandao wa Wikipedia.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited