Home Soka Lampard Hali Tete

Lampard Hali Tete

by Sports Leo
0 comments

Licha ya kukabiliwa na mchezo mgumu ugenini dhidi ya Wolves kocha wa Chelsea Frank Lampard ana wakati mgumu kutokana na mastaa takribani nane wa kikosi cha kwanza kuwa majeruhi.

Mastaa hao wakiongozwa na Ngolo Kante na Antonia Rudger ambao wamepata majeraha hivi karibuni huku beki wa kushoto Emerson naye ameongezeka baada ya kupata tatizo la misuli katika mchezo wa Italia dhidi ya Finland.

Wengine ni Callum Hudson-Odoi,Ruben Roftus Cheek,Mateo Kovacic,Pedro Rodriguez,Reece James ambao wanamatatizo mbalimbali yanayowafanya wasiwe fiti kuwavaa Wolves huku ikitarajiwa baadhi yao wanaweza kuwahi mechi hiyo japo hawawezi kupambana kwa dakika zote tisini.

banner

Chelsea imekua na mwendo wa kusuasua kutokana na kutofanya usajili wa kutosha baada ya kupewa adhabu na shirikisho la soka duniani(Fifa) ya kutosajili huku ikiwa imecheza jumla ya mechi 4 wakiwa wamecheza kwenye ligi kuu ya uingereza wakishinda moja na kufungwa moja huku mechi mbili wakitoa sare.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited