Home Soka Lomalisa Kuwakosa Medeama Fc

Lomalisa Kuwakosa Medeama Fc

by Dennis Msotwa
0 comments

Beki wa kushoto wa klabu ya Yanga sc Joyce Lomalisa anatarajiwa kuukosa mchezo wa tatu wa hatua ya makundi ya kombe la klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Medeama Fc baada ya kushindwa kupona majeraha.

Beki huyo aliumia katika mchezo wa sare ya 1-1 dhidi ya Al Ahly baada ya kukanyagwa na Percy Tau ambapo alitolewa nje kwa matibabu zaidi na nafasi yake kuchukuliwa na Nickson Kibabage ambapo sasa ripoti ya madaktari wa klabu hiyo imeonyesha kuwa bado hajapona.

Kocha Miguel Gamondi sasa inampasa kumuanzisha mmoja kati ya Nickson Kibabage,Farid Musa ama Kibwana Shomari katika eneo hilo ili kuziba nafasi ya Lomalisa anayesifika kwa kupiga krosi nzuri za ushindi.

banner

Tayari msafara wa kikosi hicho umeanza safari kuelekea nchini Ghana huku staa huyo akisalia nchini kwa ajili ya kuendelea na matibabu zaidi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited