Home Soka Lusajo Hana Presha Yanga

Lusajo Hana Presha Yanga

by Sports Leo
0 comments

Staa wa klabu ya Namungo Reliant Lusajo amesema hana presha endapo akisajiliwa na klabu ya Yanga kutokana na kuamini kiwango chake cha sasa.

Lusajo aliyewahi kusajiliwa Yanga kisha kukosa nafasi chini ya kocha Ernie Brandt kutokana na kutokua na uzoefu ambapo alijiunga na klabu mbalimbali kama Toto Afrika kisha kutua Namungo anakowika mpaka sasa.

“Nina amini kwamba uwezo wa mchezaji huwa haujifichi, iwapo nitapata nafasi ya kurejea Yanga nitaendelea na kasi yangu ya kutupia pale nitakapopata nafasi.

banner

“Uzuri ni kwamba kwa sasa nimezidi kuimarika na kuwa na uwezo wa kufunga jambo ambalo linanifanya niamini kwamba ninaweza kucheza popote ndani na nje ya Bongo,” amesema.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited