Home Soka Makambo Awaita Mashabiki

Makambo Awaita Mashabiki

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga sc Heritier Makambo amewataka mashabiki wa klabu hiyo kujitokeza kwa wingi siku ya mchezo wa hatua ya awali ya klabu bingwa dhidi ya River United utakaochezwa nchini siku ya Jumapili uwanja wa B.mkapa jijini Dar es salaam.

Mchezo huo utakofuatiwa na marudiano baada ya siku saba ni muhimu kwa Yanga sc kushinda ili kujiweka sawa kufuzu michuano hiyo na kupunguza presha kwa mashabiki baada ya timu hiyo kufungwa na timu ya Zanaco Fc katika mchezo wa siku ya kilele cha’wiki ya mwananchi kilichofanyika wiki iliyopita.

”Mashabiki mje kwa waingi siku ya jumapili tar 12,tuje kuwajaza kwa pamoja mkumbuke ninyi ni wachezaji wa 12 uwanjani.💛💚” Aliandika mshambuliaji huyo kipenzi cha mashabiki wa Yanga sc aliyejiunga akitokea Horoya Fc ya nchini Guinnea.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited