Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka nchini Uingereza Manchester City wametangazwa kuwa ndiyo timu yenye kikosi ghali zaidi duniani na jarida la kiuchumi la CIES football observatory la Ufaransa kwa mwaka 2021.
Katika dirisha la usajili lililopita mabingwa hao waliongeza thamani ya kikosi chao kwa kumsajili nahodha wa Aston Villa Jack Grealish kwa Paundi milioni 100 za Kiingereza na kuwafanya kufikia thamani ya Paundi bilioni 1.28.
Wapinzani wakubwa wa Man City klabu ya Manchester United imeshika nafasi ya pili wakiwa na kikosi chenye thamani ya Paundi bilioni 1.21 huku mabingwa watetezi wa kombe la Ulaya Chelsea wakishika nafasi ya tatu kwa Paundi milioni 808.
Orodha kamili ya vilabu vyenye vikosi ghali zaidi duniani ni kama ifuatavyo.
Â