Home Soka Man Utd Yaipiga Liverpool

Man Utd Yaipiga Liverpool

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Manchester United i8mefanikiwa kupata ushindi wa   kibabe sana katika  moja ya mechi ngumu  kwenye Kombe la FA baada ya kuifunga  Liverpool Fc kwa mabao 4-3 katika mchezo uliochezwa kwa dakika 90 na 30mza nyongezauliofanyika katika  uwanja wa Old Trafford jijini Manchester.

Man Utd chini ya kocha mdachi  Erik ten Hag ilianza kupata  bao mapema kupitia kwa  Scott McTominay dakika ya 10 ya mchezo huku Liverpool ikafunga mara mbili ndani ya dakika tatu za 44 na 45+2 na kuongoza 2-1 kabla ya mapumziko.

Wengi wakiamini kuwa Man Utd itapoteza mchezo huo, Mbrazili Antony alirudisha matumaini baada ya kusawazisha na kufanya matokeo yawe 2-2 dakika ya 87 ya mchezo na  kulazimisha mechi hiyo kuingia kwenye dakika 30 za nyongeza.

banner

Kukosekana kwa umakini kwa Man utd kulisababisha Harvey Elliott kujifungia bao jingine Liverpool dakika ya 105 lakini Man utd walisawazisha kupitia kwa  Marcus Rashford dakika ya 112 huku Amad Diallo kufunga bao la nne kwenye dakika 120 na hivyo Man United kupinga nusu fainali ya Kombe la FA kibabe.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited