Home Soka Man Utd,Arsenal Hawachekani

Man Utd,Arsenal Hawachekani

by Sports Leo
0 comments

Ni kama wana ugonjwa mmoja baada ya wote kuambulia sare katika michezo ya ligi kuu nchini Uingereza na kuzidi kudidimiza matumaini ya kumaliza katika nafasi ya nne bora.

United ilibanwa na Aston Villa ambao walitangulia kupata bao la mapema dakika ya 11 likifungwa na Jacky Grealish ambalo lilisawazishwa na Tom Heaton kwa kujifunga na victor Lindelof aliongeza bao la pili dakika ya 64 lililodumu kwa dakika 2 baada ya Tyrone Mings kusawazisha dakika ya 66.

Matokeo hayo yanaifanya United isalie nafasi ya 9 ikiwa na pointi 18 huku Arsenal waliotoka sare na Norwich wakisalia nafasi ya 8 na pointi 19.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited