Taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba sc imeonyesha kumteua Ezekiel Kamwaga kuwa kaimu mkuu wa Idara ya Habari ya klabu hiyo kuchukua nafasi ya Haji Manara ambae bodi imeridhia ombi lake la kujiuzuru nafasi hiyo ya pendwa na mashabiki wa klabu hiyo.
Kwa mujibu wa barua hiyo Kamwaga ambae ni mwandishi wa habari mkongwe atakua na jukumu la kufumua Idara hiyo ili kutengeneza muundo mpya wa idara hiyo ili kuleta ufanisi katika kipindi hicho kisha klabu itatangaza nafasi za kazi rasmi.