Home Soka Manula,Kakolanya Watemwa Stars

Manula,Kakolanya Watemwa Stars

by Sports Leo
0 comments

Makipa wa klabu ya Simba sc Aishu Manula na Beno Kakolanya wameachwa katika kikosi cha timu ya taifa (Taifa stars) kilichochaguliwa kwa ajili ya mchezo wa kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) dhidi ya Sudan.

Kikosi hicho kitachoongozwa na kaimu kocha mkuu Ettiene Ndayiragije na wasaidizi Juma Mgunda na Seleman Matola kimetangazwa huku nafasi za makipa hao zikichukuliwa na Juma Kaseja na Metacha Mnata ambao wamekua na viwango vizuri siku za karibuni.

banner

Pia katika kikosi hicho wachezaji Mzamiru Yassini na Miraji Athuman kutoka Simba sc wameitwa kufuatia kufanya vizuri katika michezo ya klabu yao huku Miraji akiwa amecheza michezo miwili na kufunga mabao mawili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited