Makipa wa klabu ya Simba sc Aishu Manula na Beno Kakolanya wameachwa katika kikosi cha timu ya taifa (Taifa stars) kilichochaguliwa kwa ajili ya mchezo wa kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) dhidi ya Sudan.
Kikosi hicho kitachoongozwa na kaimu kocha mkuu Ettiene Ndayiragije na wasaidizi Juma Mgunda na Seleman Matola kimetangazwa huku nafasi za makipa hao zikichukuliwa na Juma Kaseja na Metacha Mnata ambao wamekua na viwango vizuri siku za karibuni.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Pia katika kikosi hicho wachezaji Mzamiru Yassini na Miraji Athuman kutoka Simba sc wameitwa kufuatia kufanya vizuri katika michezo ya klabu yao huku Miraji akiwa amecheza michezo miwili na kufunga mabao mawili.