Home Soka Mapokezi Ntibanzokiza Usipime

Mapokezi Ntibanzokiza Usipime

by Sports Leo
0 comments

Jana mashabiki wa klabu ya Yanga sc waliendeleza utamaduni wao wa kuwapokea mastaa wa timu hiyo wakimpokea mshambuliaji Saido Ntibanzokiza akitokea nchini Burundi kuja kujiunga na timu hiyo baada ya kusajiliwa wiki kadhaa nyuma.

Saido ni mmoja kati ya wachezaji wenye uzoefu mkubwa akiwa amecheza vilabu kadhaa barani ulaya ikiwemo kucheza katika ligi ya Ufaransa hivyo wanayanga wana matumaini makubwa kwa staa huyo atamaliza ukame wa mabao klabuni hapo.

Mapokeza ya mchezaji huyo yaliongozwa na makamu mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo Eng.Hersi Said akiwa na Mkuu wa Idara ya Habari Hassan Bumbuli pamoja naAfisa Hamasa Antonio Nugaz huku mashabiki wakijitokeza kama ilivyo kawaida yao

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited