Home Soka Mastaa Arsenal Kukatwa Mshahara

Mastaa Arsenal Kukatwa Mshahara

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji wa Arsenal, wamekubali kukatwa asilimia 12.5 ya mishahara yao, baada ya kuahidiwa ‘bonasi’ kubwa katika ligi ya mabingwa Ulaya na kombe la ligi ya Europa.

Wachezaji watafidia fedha watakazokatwa kwa kila mmoja kulipwa pauni laki moja (£100,000), endapo watafuzu kucheza msimu ujao wa ligi ya mabingwa ya Ulaya.

Klabu pia, imeahidi kumlipa kila mchezaji bonasi ya pauni laki tano (£500,000) kama watatwaa taji la ligi ya mabingwa Ulaya mwaka 2021 au pauni laki moja (£100,000) kama wataibuka mabingwa wa ligi ya Europa.

banner

Arsenal, imekuwa klabu ya kwanza ya ligi kuu England, kukubali mpango wa kukata mishahara kwa wachezaji wake, katika kipindi hiki ambacho klabu nyingi duniani zimeathirika kiuchumi kutokana na janga la virusi vya Corona.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited