Home Soka Matola Huyoo Simba

Matola Huyoo Simba

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha wa timu ya Polisi Tanzania Selemani Matola anaelekea kujiunga na timu ya Simba sc baada ya kuomba kuvunja mkataba na timu hiyo ambayo makao makuu yake yako mkoani Kilimanjaro nchini.

Matola anatajwa kwenda Simba kuchukua nafasi ya kocha Dennis Kitambi ambaye anaondolewa baada ya klabu hiyo kuamua kuvunja benchi lote la ufundi huku ikiwa tayari imempa mkono wa kwaheri kocha mkuu Patrick Aussems.

“Kwa sasa tunashughulikia ombi lake la kuvunja mkataba maana lina hatua kadhaa za kuzifuata na tukimaliza ndio tutajadili majina yaliyopendekezwa mezani juu ya nani awe kocha msaidizi”.Alisema Frank Godfrey kaimu katibu mkuu wa timu hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited