Kocha wa timu ya Polisi Tanzania Selemani Matola anaelekea kujiunga na timu ya Simba sc baada ya kuomba kuvunja mkataba na timu hiyo ambayo makao makuu yake yako mkoani Kilimanjaro nchini.
Matola anatajwa kwenda Simba kuchukua nafasi ya kocha Dennis Kitambi ambaye anaondolewa baada ya klabu hiyo kuamua kuvunja benchi lote la ufundi huku ikiwa tayari imempa mkono wa kwaheri kocha mkuu Patrick Aussems.
“Kwa sasa tunashughulikia ombi lake la kuvunja mkataba maana lina hatua kadhaa za kuzifuata na tukimaliza ndio tutajadili majina yaliyopendekezwa mezani juu ya nani awe kocha msaidizi”.Alisema Frank Godfrey kaimu katibu mkuu wa timu hiyo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.