Home Soka Mbao Wagoma Kuingia Kambini

Mbao Wagoma Kuingia Kambini

by Sports Leo
0 comments

Licha ya uongozi wa klabu ya Mbao fc kuwaita wachezaji wake kambini kujiandaa na michezo ya ligi kuu iliyosalia taarifa zkutoka klabuni hapo zinadai hakuna mchezaji hata mmoja aliyeripoti kambini.

Klabu hiyo wenyeji wa jiji la Mwanza maeneo ya sabasaba wameiomba bodi ya ligi (TPLB) na Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kuikopesha pesa klabu hiyo ili iweze kumudu gharama za kuiweka kambi timu jijini Dar es salaam kumalizia michezo iliyosalia.

Awali serikali kupitia kwa Waziri mwenye dhamana ya Michezo nchini Dk.Harrison Mwakyembe aliweka wazi kuwa michezo yote iliyosalia ya ligi kuu itachezwa jijini Dar es salaam ili kuepuka maambukizi ya Virusi vya Corona ambapo timu zitapaswa kuweka kambi katika jiji hilo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited