Home Soka Mbaya Wa Simba Kutua Yanga

Mbaya Wa Simba Kutua Yanga

by Sports Leo
0 comments

Yule mbaya wa Simba aliyewaua katika mechi ya kimataifa dhidi ya Ud Songo Luis Jose Miqquisone ananyemelewa na Yanga katika usajili wa dirisha dogo la hivi sasa.

Staa huyo aliacha kilio uwanja wa taifa baada kufunga bao liliitoa rasmi Simba kwenye michuano ya kimataifa hadi kusababisha imani ya viongozi na mashabiki wa klabu hiyo kwa kocha Patrick Aussems kupungua kwa kiasi kikubwa tayari yupo kwenye rada za jangwani na tayari mchakato wa kumtumia tiketi ya ndege umeanza.

Staa huyo ni mali ya Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini na kama rada zitaa sawa anaweza kutua Jangwani kama mchezaji huru baada ya kuonyesha nia ya kuvunja mkataba na klabu yake ya Mamelods ambayo humtoa kwa mkopo mara kwa mara.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited