Mshambuliaji wa Kagera sugar Yusuph Mhilu amejiunga na mabingwa watetezi wa ligi kuu bara klabu ya soka ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili.
Mchezaji huyo aliyefunga mabao 9 msimu huu amejiunga Simba sc akiwa mchezaji huru.
Mhilu aliwahi kucheza kwa wapinzani wa jadi wa Simba klabu ya soka ya Yanga msimu wa 2018/2019 kabla ya kujiunga na Kagera alikocheza kwa mafanikio.